• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi & Mipango Miji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Taka Ngumu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uchumi
      • Utawala & Rasilimali Watu
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Matumizi bora ya Ardhi
    • Miundombinu yetu
    • Viwanda
    • Biashara
    • Utalii
    • Rasilimali za mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Huduma ya Maji
    • Education
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • UKIMWI
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

Matumizi bora ya Ardhi

MRADI WA UPIMAJI NA UUZAJI WA  VIWANJA 2000 ENEO LA NAMBOGO NA KATUMBA AZIMIO 

UTANGULIZI:

Mradi wa upimaji viwanja Nambogo  na Katumba Azimio  umetekelezwa kwa ubia kati ya Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga na Mfuko wa Mafao ya Kustaafu (GEPF), hii itasaidia upatikanaji wa viwanja vilivyopimwa na kuwekewa miundombinu ya msingi  na kusogeza huduma mbalimbali kwa wananchi waishio katika kata za pembezoni za Pito, Molo, Milanzi, Lwiche nk.

Utekelezaji wa mradi huu utasaidia kupunguza ujenzi holela, unaosababishwa na ongezeko la watu. Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ilikuwa na watu 209,793 sawa na ongezeko la asilimia 43 % ya idadi wa watu 146,842 katika sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002.

Ongezeko hili la watu limesababisha ujenzi holela na usio na huduma za kijamii na kiuchumi kwa sababu miji mingi haikujiandaa kupokea idadi hiyo kubwa kwa ajili ya kuwapatia makazi na huduma zingine.

Aidha tafiti nyingi zinaonesha ukuaji huu wa kasi wa miji hauendi sambamba na upatikanaji wa huduma za kijamii na kiuchumi kama shule huduma za afya, maji, barabara, umeme miundombinu ya uzoaji taka n.k.

Jitihada mbalimbali zimeanza kuchukuliwa na Halmashauri kuweza kukabiliana na suala la upatikanaji wa viwanja vilivyopimwa kwa kutafuta wabia kutoka taasisi za umma na binafsi na pia kuzungumza na wamiliki wa ardhi kuingia makubaliano ya kupima viwanja na kisha kugawana asilimia ya viwanja vitavyozalishwa.

 

LENGO LA MRADI

Lengo kuu la mradi huu wa Nambogo ni kuwa na mji wa kisasa utakaokuwa na huduma mbalimbali ili kupunguza msongamano wa kufuata huduma katika eneo la kitovu cha mji (Central Business District) kwa siku za usoni. Sambamba na hilo, mradi utasaidia kuongeza upatikanaji wa viwanja vilivyopimwa na kuwekewa miundo mbinu ya msingi, hivyo kupunguza kasi ya ujenzi holela.

 

GHARAMA YA MRADI

Gharama za mradi zilizotumika Tshs. 1,589,692,000, ambazo kati ya hizo kiasi cha Tshs. 1,536,305,000, kimetolewa na GEPF na kiasi cha Tshs. 53,387,000 kimetolewa na Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga.

Aidha Manispaa imetoa usimamizi wa kila siku wa mradi, wataalamu na ofisi kwa ajili ya uendeshaji wa mradi.

Uthamini na malipo ya fidia kwa wananchi 155 wenye ardhi umeshafanyika na kupewa stahiki zao kwa kupitia Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga```

 

FAIDA YA MRADI 

  • Kuwa na mji uliopangwa na wenye miundo mbinu ya msingi na unaopendekeza
  • Kuongeza upatikanaji  wa viwanja vilivyopimwa
  • Kupunguza ujenzi holela
  • Kupunguza msongamano katika eneo la kati  ya mji kwa kusogeza huduma mbalimbali katika eneo la mradi.
  • Kujenga uwezo kwa Halmashauri ili kupanga na kupima maeneo mengine kwa ajili ya kuzuia ujenzi holela.
  • Kuongeza mapato  ya Serikali kwa njia ya kodi mbalimbali
  • Kuongeza uzalishaji/mapato miongoni mwa wananchi kutokana na shughuli za kiuchumi zitakazoanzishwa katika eneo la mradi.

Jedwali: viwango vya matumizi ya viwanja.

Na 
Aina ya matumizi
Gharama kwa kila mita ya mraba
1
Makazi pekee (ujazo wa juu, kati na chini

2,700/=

2
Makazi na biashara

3,000/=

3
Biashara

5,000/=

4
Huduma za jamii

3,500/=

5
Ibada/ kuabudu

3,500/=

6
Hoteli, vituo vya mafuta na maduka ya kuiwekezaji

5,000/=


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo(aliyeshika ramani kushoto shati nyeusi na weupe) alipokwenda kutembelea Mradi wa Nambogo kujua maendeleo ya mradi huo akioneshwa namna mji huo utakavyokuwa kwenye ramani na afisa mipango miji wa Manispaa ya Sumbawanga Colman.

Eneo la Nambogo ndani ya Manispaa ya Sumbawanga lililopimwa viwanja kwaaajili na makazi na uwekezaji mbalimbali wa huduma za kijamii 

ENEO LA VIWANDA NA MAGHALA “KANONDO INDUSTRIAL AREA”

Kanondo ni eneo ambalo limetengwa kwa matumizi ya viwanda vidogo. Eneo hili lina ukubwa    mita za mraba 773,039 lipo  kando ya barabara ya kwenda Mpanda.

Katika eneo hili lipo maeneo ambayo hayatauzwa ni pamoja na barabara, maeneo ya matumizi ya umma na viwanja 9 ambavyo vilitumika katika kuchangia gharama ya  mchoro ili kuidhinishwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi.

Ukubwa wa eneo litakalouzwa

Eneo litakalouzwa litakuwa na mita za mraba 553,422.00  sawa na ekari 136.7 lenye viwanja 153

Bei elekezi ya viwanja ilitolewa na Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Kanda ya Kusini Magharibi tarehe 01/11/2016 kuwa ni Tsh. 3000/= kwa mita moja ya mraba (M2).  

MPANGO KABAMBE (MASTER PLAN) 2015 – 2035 WA MIPANGO MIJI

Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ilikuwa na Mpango Kabambe wa Miaka 20 kuanzia mwaka 1989 – 2009.  Mwaka 2010 ulianza mchakato wa kuandaa mpango Kabambe wa miaka 20.  Mchakato huo ulianza kwa hatua za awali mwaka 2011 za kuandaa Mpango Kabambe wa miaka 20 kama zinavyoainishwa  kwenye sheria ya Mipango Miji  Na. 8 ya mwaka 2007 kifungu cha 8 eneo la Mipango miji lilitagazwa kwenye gazeti la Serikali Na. 223 ya tarehe 05/8/2011.

Hatua iliyofikiwa kwenye maandalizi ya Mpango Kabambe ni kukamilisha uandaaji wa taarifa (Rasimu) ya mwisho ya Mpango Kabambe ya kuwasilisha kwa Katibu Tawala wa Mkoa ili aupitishe uwasillishwe kwa Mkurugenzi wa Mipango Miji wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.  Aidha kazi hii inatarajiwa kukamilika mwezi Machi, 2018.

Ombi kwa Wawekezaji 

Wahi nafasi za kuwekeza katika Manispaa ya Sumbawanga, Mji ambao umepania kujipanga kisasa na kuleta mvuto wa miji inayoendelea kukua nchini, Manispaa ya Sumbawanga ndio makao makuu ya Mkoa wa Rukwa ambapo inaunganisha Mkoa wa Katavi na Songwe huku ikipakana na nchi ya Zambia na Congo kwa Upande wa Ziwa Tanganyika. 


Matangazo

  • Waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 December 18, 2020
  • Walichaguliwa Kidato cha Kwanza 2021 -PDF December 18, 2020
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA. December 07, 2019
  • JOINING INSTRUCTION-LUKANGAO SECONDARY SCHOOL-MANISPAA YA SUMBAWANGA January 05, 2021
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • Mitihani Kidato cha Nne 2020

    November 23, 2020
  • MBUNGE

    March 03, 2020
  • DC

    February 13, 2020
  • WASIOPITIA JKT WATAKIWA JESHINI KATIKA UTUMISHI WAO

    September 16, 2019
  • Angalia zote

Video

Mkurugenzi aondoa sintofahamu kuhusu Sumbawanga mpya
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: 0784519681

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa